ALIANZA UJAMBAZI AKIWA NA MIAKA KUMI, JAMBAZI SUGU KUTOKA INDIA
Swahili Prime Ent Anaitwa Koose Munisamy Veerappan raia wa India aliyezaliwa 18 January 1952. Unaambiwa India waliwahi kutokea majambazi sugu na kudhibitiwa, lakini huyu ndio alikuwa kiboko. Alifanya shughuli za uhalifu kwa miaka 42 kabla ya kudhibitiwa na kuuwawa Oktoba 18, 2004 akiwa na miaka 52. Veerappan ni nani? Kila kitu kumhusu yeye kipo hapa Veerappan aliyezaliwa huko Coimbatore, India alianza kazi yake ya uhalifu tangu akiwa na umri wa miaka 10 kwa msaada wa mjomba wake Saalvai Gounder, walikuwa wanauwa tembo na kuvuna pembe za ndovu na kuuza kimagendo huku makazi yao makubwa yakiwa misituni, na baada ya muda alitengana na mjomba wake na kuanza kujitegemea. Rekodi inaonyesha kuwa katika wakati wake wote kama muhalifu 1962–2004 ameuwa zaidi ta Tembo 900, lakini ukweli ni kwamba ameuwa kati ya tembo 2000 - 3000, ameuwa watu 184 wakiwepo askari 97 na maafisa wa misituni huku akiigharimu serikali ya India zaidi ya $ 330 milioni kufanikisha kumtia nguvuni (zaidi ya TZS Bilion ...