Mwaka 1989 Kundi Hatari la Kihalifu la Medellin Cartel la Colombia Linalomilikiwa na Pablo Escobar Lililipua Ndege na Kuuwa Abiria Wote 107, Lengo Lao Lilikuwa ni Kumuua Mgombeaji Urais wa Nchi Hiyo Álvaro Gómez
Mei 27, 1990 ulifanyika uchaguzi mkuu nchini Colombia huku wagombea urais wakiwa ni César Gaviria wa chama cha Liberal na mpinzani wake Álvaro Gómez Hurtado wa chama cha MSN, Cesar alipita kwa asilimia 48% za kura na kuwa rais wa 28 wa Colombia. Katika kampeni zilizoanza tangu mwaka 1989, mgombea Alvaro alikuwa akitumia sera ya kutokomeza biashara ya dawa za kulevya nchini humo akidai kuwa serikali ya awamu iliyopita imekuwa ikishirikiana na makundi makubwa ya dawa za kulevya hivyo yeye akichaguliwa kuwa rais atakomesha biashara hiyo haramu. Moja ya makundi hatari ya biashara hio nchini humo ni Medellin Cartel linalomilikiwa na mtu m'bad Pablo Escobar, walivyosikia ngebe hizo mipango ya kutoa uhai wa mgombea huyo ikaanza. Taarifa zilizowafikia wauza unga hao ni kwamba Alvaro alitarajia kusafiri siku ya November 27, 1989 kutoka Bogotá kwenda Soacha kwa usafiri wa ndege ya shirika la ndege la Boeing 727, Avianca Flight 203, ndipo walipanga kuilipua ndege hiyo ili kumteketeza mgombea...