Posts

Mwaka 1989 Kundi Hatari la Kihalifu la Medellin Cartel la Colombia Linalomilikiwa na Pablo Escobar Lililipua Ndege na Kuuwa Abiria Wote 107, Lengo Lao Lilikuwa ni Kumuua Mgombeaji Urais wa Nchi Hiyo Álvaro Gómez

 Mei 27, 1990 ulifanyika uchaguzi mkuu nchini Colombia huku wagombea urais wakiwa ni César Gaviria wa chama cha Liberal na mpinzani wake Álvaro Gómez Hurtado wa chama cha MSN, Cesar alipita kwa asilimia 48% za kura na kuwa rais wa 28 wa Colombia. Katika kampeni zilizoanza tangu mwaka 1989, mgombea Alvaro alikuwa akitumia sera ya kutokomeza biashara ya dawa za kulevya nchini humo akidai kuwa serikali ya awamu iliyopita imekuwa ikishirikiana na makundi makubwa ya dawa za kulevya hivyo yeye akichaguliwa kuwa rais atakomesha biashara hiyo haramu. Moja ya makundi hatari ya biashara hio nchini humo ni Medellin Cartel linalomilikiwa na mtu m'bad Pablo Escobar, walivyosikia ngebe hizo mipango ya kutoa uhai wa mgombea huyo ikaanza. Taarifa zilizowafikia wauza unga hao ni kwamba Alvaro alitarajia kusafiri siku ya November 27, 1989 kutoka Bogotá kwenda Soacha kwa usafiri wa ndege ya shirika la ndege la Boeing 727, Avianca Flight 203, ndipo walipanga kuilipua ndege hiyo ili kumteketeza mgombea...

ALIANZA UJAMBAZI AKIWA NA MIAKA KUMI, JAMBAZI SUGU KUTOKA INDIA

 Swahili Prime Ent Anaitwa Koose Munisamy Veerappan raia wa India aliyezaliwa 18 January 1952. Unaambiwa India waliwahi kutokea majambazi sugu na kudhibitiwa, lakini huyu ndio alikuwa kiboko. Alifanya shughuli za uhalifu kwa miaka 42 kabla ya kudhibitiwa na kuuwawa Oktoba 18, 2004 akiwa na miaka 52. Veerappan ni nani? Kila kitu kumhusu yeye kipo hapa Veerappan aliyezaliwa huko Coimbatore, India alianza kazi yake ya uhalifu tangu akiwa na umri wa miaka 10 kwa msaada wa mjomba wake Saalvai Gounder, walikuwa wanauwa tembo na kuvuna pembe za ndovu na kuuza kimagendo huku makazi yao makubwa yakiwa misituni, na baada ya muda alitengana na mjomba wake na kuanza kujitegemea. Rekodi inaonyesha kuwa katika wakati wake wote kama muhalifu 1962–2004 ameuwa zaidi ta Tembo 900, lakini ukweli ni kwamba ameuwa kati ya tembo 2000 - 3000, ameuwa watu 184 wakiwepo askari 97 na maafisa wa misituni huku akiigharimu serikali ya India zaidi ya $ 330 milioni kufanikisha kumtia nguvuni (zaidi ya TZS Bilion ...

SIMBA WALIOKWAMISHA UJENZI WA RELI KWA MWAKA MZIMA

 Swahili Prime Ent Kwa Mujibu wa Taarifa ya Uchunguzi, Mwaka 1898 Simba Wawili Wakali Walidaiwa Kutumwa Kwa Makusudi ili Wakawauwe Wafanyakazi Waliokuwa Wanajenga Reli ya Kenya - Uganda na Kukwamisha Ujenzi Huo kwa Karibia Mwaka Mzima. Simba Hao Wanadaiwa Kuwala Wafanyakazi 140. Katikati ya machi 1898 usiku, wafanyakazi katika mradi wa reli ya Uganda, ambayo inaunganisha na Kenya, walishambuliwa na simba wawili na kuibuka mauaji ya kutisha zaidi ya mnyama kuwashambulia binadamu katika historia. Iweje itajwe kuwa simba walitumwa? Madhara na mwisho wake ulikuwaje?  Inaelezwa kuwa Machi 1898 simba wawili waliwavamia wafanyikazi usiku wa manane katika kambi yao na kusababisha vifo vya wafanyikazi 140 wa Kiafrika na Wahindi, na iliainishwa kama mauaji mabaya zaidi kufanywa na mnyama dhidi ya wanadamu katika historia. Lakini nyuma ya pazia inaelezwa kuwa sababu ya mauaji hayo ni simba hao kutumwa, kusogezwa makusudi karibu na mradi ili wawashambulie wafanyakazi kwasababu wahusika wa...

MFUNGWA HATARI ALIYETOROKA GEREZANI KWA KUTUMIA UZI!

 Swahili Prime Ent: Mfungwa Robert Dale Shepard Raia wa US Aliyetumia Kamba za Kusafishia Meno Kutoroka Katika Gereza la South Central Regional Jail Virginia kwa Kukwea Ukuta wa Futi 18 Mwaka 1994. Alifuma Kamba ya Futi 20. June 29, 1994 mfungwa Robert Dale Shepard (34) aliyekuwa anatumikia kifungo katika gereza moja mashariki mwa Virginia US, alifanikiwa kutoroka gerezani kwa kupanda ukuta akitumia kamba nyembamba ya kusafishia meno. Inaelezwa kuwa baada ya kutoroka alitumia siku 41 kuishi msituni, akiishi kwa matunda na kuoga kwenye mito, hadi alipokamatwa tena akiwa amenyooshewa bunduki na askari baada ya kudaiwa kuiba duka la dawa karibu na mji wake wa Parkersburg. Shepard alikuwa akikusanya kamba ndogo kwa miezi mingi zilizokuwa zinagawiwa kwa wafungwa ili kusafishia meno gerezani hapo, akaunganisha na kufuma kamba moja ndefu na imara iliyomsaidia kutoroka kupitia ukuta wa gereza wa futi 18. Katika mahojiano yake baada ya kukamatwa Shepard alisema kua kabla ya jaribio lake ku...

Anaitwa Chris McCandless Raia wa California US. Mwaka 1992 Akiwa na Miaka 24 Aliamua Kuingia Porini, Mbali ili Akaishi Maisha ya Asili, Maisha Kama ya Wanyama kwa Miezi 3 Kisha Arudi Nyumbani. Miezi Mitatu Baadaye Mwili Wake Ulipatikana Umeoza Porini. Inaelezwa Alikufa kwa Njaa.

Majina yake halisi anaitwa Christopher Johnson McCandless mzaliwa wa California US. Kwa hiyari yake mwenyewe katikati ya mwaka 1992 akiwa na miaka 24 aliamua kutoka nyumbani kwake na kuingia porini mbali huko Alaska ili kujipatia uzoefu wa maisha mapya ya asili yasiyowategemea binadamu wengine. Chriss Aliingia porini kupata uzoefu wa kuishi maisha kama mnyama wa porini, alipanga kuishi huko kwa miezi mitatu na kurejea nyumbani huku akibeba notebook ya kuandika vidokezo pamoja na camera ndogo. Taarifa zinasema kuwa Chris alikufa miezi mitatu baadae Agosti 18, 1992, ikiwa ni siku ya 112 baada ya kutembea porini. Mwili wake ulipatikana siku 19 baadaye pamoja na notebook yake na camera. Kuna uwezekano mkubwa kwamba Chriss alikufa kutokana na njaa na utapiamlo. Chris alitaka kuishi kiasili akiwa porini kwa miezi michache. Kweli baada ya miezi mitatu huko porini alianza safari ya kurudi nyumbani lakini alipofika mto Teklanika alikuta mto umejaa maji mengi kiasi cha kushindwa kuvuka. Kati...

SIRO NZITO:JINSI FAMILIA YA GLAZER ILIVYOICHUKUA MANCHESTER UNITED KIMAFIA NA KUIINGIZA KWENYE MADENI MAKUBWA!

Swahili Prime Ent Leo tunaitazama historia ya kushtua ya jinsi bilionea Malcolm Glazer alivyofanikisha ununuzi wa Manchester United kati ya mwaka 2003 na 2005. Huu ulikuwa ununuzi uliogubikwa na malalamiko mengi ambayo hadi leo yamesababisha vuguvugu la Glazers Out. Hatua kwa Hatua ya Ununuzi: 1. Mwanzo Mdogo (Machi 2003): Malcolm Glazer alianza kwa kununua hisa ndogo tu ya 2.9% kwa takriban pauni milioni 9 (£9M). Wakati huo, United ilikuwa kampuni iliyoorodheshwa kwenye soko la hisa. 2. Ujanja wa Soko la Hisa:Kwa kipindi cha miaka miwili, Glazer aliendelea kununua hisa kidogo kidogo sokoni hadi akafikia kiwango cha kuanza kuidhibiti klabu. 3. Mapinduzi ya Mwaka 2005: Mwezi Mei 2005, familia ya Glazer ilikamilisha ununuzi wa karibu 98% ya klabu kwa thamani ya pauni milioni 790 (£790M). Kwanini Mashabiki Walikasirika? (Leveraged Buyout): Hapa ndipo penye siri ya madeni ya United. Glazer hakutumia pesa yake yote mfukoni. Badala yake: Alikopa kiasi kikubwa cha fedha (takriban pauni milion...

MWANAMKE ALIYETABIRI MAMBO YANAYOTIMIA HADI WAKATI HUU

 Swahili Prime Ent: Moja ya Utabiri Aliouacha Baba Vanga Raia wa Bulgaria, Mmoja wa Watabiri Maarufu Kutokea Alisema Kuwa Kuanzia Mwaka 2023 Itakua ni Kawaida tuu kwa Mwanake Kwenda Maabara Kupandikizwa Mtoto na Baadaye Kuzaa. Alifariki Mwaka 1996 Akiacha Tabiri Zaidi ya 100, na Nyingizo Zinatimia.   Baba Vanga ni Nani? Baba Vanga alikuwa mwanamke kipofu ambaye aliacha ubashiri kwa kila mwaka hadi mwaka 5079. Alizaliwa Vangelia Pandeva Dimitrova Bulgaria.  Alipokuwa na umri wa miaka 12, dhoruba ilimpiga na kumfanya apotee katika machafuko hayo na kupoteza uwezo wake wa kuona. Alipatikana siku chache baadaye akiwa kipofu. Baba Vanga alidai kuwa alipata maono yake ya kwanza katika siku alizopotea na kimbunga hicho, na baadaye alisema uwezo wake wa kuona umebadilishwa, badala ya kuona kawada yeye anaweza kuona siku zijazo. Alifariki mwaka 1996 (85). BAADHI YA UTABIRI WAKE ULIOTIMIA. 1️⃣Mwaka 1989 Vanga alisema: "Waamerika wataanguka baada ya kushambuliwa na ndege w...