KUTOKA KUZIMIA HADI USHINDI: Safari ya Eric Chelle Inayofundisha Dunia!

Katika soka, kuna wakati maumivu yanakuwa makubwa kuliko uwezo wa binadamu kustahimili. Huu ulikuwa ukweli mchungu kwa kocha Eric Chelle wakati wa mashindano ya AFCON 2023.


Wengi hawatasahau picha ya kocha huyu akimwagiwa maji kichwani baada ya kukaribia kuzimia kwa presha (stress) wakati timu yake ya Mali ikipoteza dhidi ya Ivory Coast. Dunia ilimcheka, na muda mfupi baadaye, serikali ya Mali ilimfuta kazi.

Lakini kama wasemavyo, "Simba akivizia, hadhara hudhani ni mgonjwa." Leo hii, Eric Chelle amerejea kileleni akiinoa timu ya Taifa ya Nigeria, Super Eagles. Chini ya uongozi wake katika mashindano ya AFCON 2025, Nigeria imeonekana kuwa tishio, ikicheza soka la kasi na lenye nidhamu.

Safari ya Chelle inatufundisha kuwa:

* Kushindwa kwa leo siyo mwisho wa maisha.

* Watu wanaokucheka leo, watakupongeza kesho ukikataa kukata tamaa.

* Afya ya akili na presha ni vitu halisi katika kazi yoyote ile.


Comments

Popular posts from this blog

Mwaka 1989 Kundi Hatari la Kihalifu la Medellin Cartel la Colombia Linalomilikiwa na Pablo Escobar Lililipua Ndege na Kuuwa Abiria Wote 107, Lengo Lao Lilikuwa ni Kumuua Mgombeaji Urais wa Nchi Hiyo Álvaro Gómez

ALIKATWA MKONO, LAKINI HAIKUMZUIA KUCHEZA MPIRA KWA MAFANIKIO MAKUBWA!

Anaitwa Chris McCandless Raia wa California US. Mwaka 1992 Akiwa na Miaka 24 Aliamua Kuingia Porini, Mbali ili Akaishi Maisha ya Asili, Maisha Kama ya Wanyama kwa Miezi 3 Kisha Arudi Nyumbani. Miezi Mitatu Baadaye Mwili Wake Ulipatikana Umeoza Porini. Inaelezwa Alikufa kwa Njaa.