🚨 BREAKING: Michael Carrick Arejea Nyumbani! Ameshinda Vita dhidi ya Solskjaer Kurithi Mikoba Man Utd! 🔴👀

SWAHILI PRIME ENT, Manchester: Ile sintofahamu ya nani atakuwa kocha wa muda wa Manchester United inakaribia kufikia kikomo. Taarifa za hivi punde zinasema kuwa klabu hiyo imekuwa na mazungumzo yenye mafanikio makubwa na kiungo wao wa zamani, Michael Carrick.


Carrick anaonekana kuwa mbele ya kocha mwingine wa zamani, Ole Gunnar Solskjaer, na yuko tayari kukubali jukumu hilo la kuiongoza timu katika kipindi hiki cha mpito.


Kwanini Carrick?

* Anaijua vizuri falsafa ya klabu.

* Alionyesha uwezo mkubwa alipokuwa kaimu kocha hapo awali kabla ya kwenda kuinoa Middlesbrough.

 Mashabiki na wachezaji wana imani kubwa naye.


Manchester United inatarajia kumtangaza kocha huyo mpya ndani ya saa 24 hadi 48 zijazo mara tu taratibu za mwisho zitakapokamilika.

Na anatarajiwa kuiongoza timu kwenye Manchester derby, mchezo utakaochezwa Juma mosi trh 17 pale Old Trafford

Comments

Popular posts from this blog

Mwaka 1989 Kundi Hatari la Kihalifu la Medellin Cartel la Colombia Linalomilikiwa na Pablo Escobar Lililipua Ndege na Kuuwa Abiria Wote 107, Lengo Lao Lilikuwa ni Kumuua Mgombeaji Urais wa Nchi Hiyo Álvaro Gómez

ALIKATWA MKONO, LAKINI HAIKUMZUIA KUCHEZA MPIRA KWA MAFANIKIO MAKUBWA!

Anaitwa Chris McCandless Raia wa California US. Mwaka 1992 Akiwa na Miaka 24 Aliamua Kuingia Porini, Mbali ili Akaishi Maisha ya Asili, Maisha Kama ya Wanyama kwa Miezi 3 Kisha Arudi Nyumbani. Miezi Mitatu Baadaye Mwili Wake Ulipatikana Umeoza Porini. Inaelezwa Alikufa kwa Njaa.